Hamisa Hassan Mobeto ambaye ni model na actress anayekimbiza katika tasnia ya filamu nchini anadaiwa kuwa mapenzini na Diamond Platinumz a.k.a Sukari ya warembo huku uhusiano wao ukidaiwa kuwa wa muda mrefu.....
Chanzo kimoja kilichodai kuwa karibu na Hamisa ambaye alishawahi kushiriki katika mashindano ya Miss Tanzania kiliuambia mtandao wa Swahiliworld kuwa Hamisa na Diamond ni wapenzi wa muda mrefu na kwamba Wema Sepetu hana lake kwa Diamond:
"Hivi mnajua kuwa Diamond anawachanganya kwa wakati mmoja Wema na Hamisa Mobeto?, Hamisa na Diamond ni wapenzi wa muda mrefu sana lakini wanafanya siri...Hamisa anamwangalia tu Wema akiwewesekea penzi la Diamond huku yeye akijilia kivyake".Kilisema chanzo hicho
Hamisa alipotafutwa ili kutolea ufafanuzi madai hayo hakuweza kupatikana mara moja.
No comments:
Post a Comment