Wednesday 5 June 2013

UTAFITI: WATU WEUSI NDIYO WANAONGOZA KWA UNENE

 

Utafiti uliofanywa na Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Centers for Disease Control and Prevention) vya Marekani unaonyesha kwamba watu weusi ndiyo wanaongoza kwa unene wa futufutu (obesity) hapa Marekani. Utafiti huo umeonyesha kwamba karibia asilimia 36 ya watu weusi ni wanene futufutu ikilinganishwa na asilimia 24 tu kwa wazungu. Hii ni hatari kwa sababu unene huu wa futufutu ndiyo kisababishi kikubwa cha magonjwa kama kisukari (diabetes), magonjwa ya moyo, kiharusi, shinikizo la damu na baadhi ya saratani. Hii pengine inaweza kueleza ni kwa nini watu weusi ndiyo wanaongoza kwa kufa mapema hapa Marekani.

Sababu kubwa iliyotajwa katika utafiti huu ni umasikini. Watu weusi ndiyo masikini zaidi na kwa hivyo hawana pesa za kujinunulia vyakula vizuri visivyonenepesha (kama mbogamboga), bima za afya na pesa za kujiunga na vilabu vya kufanyia mazoezi (gyms).

Sababu zingine ni za kitamaduni. Imetajwa kwa mfano kwamba katika utamaduni wa watu weusi unene (ukiwemo huu wa futufutu) hauonwi kama ni tatizo na kwa hivyo watu hawaoni sababu za kujibidisha kupunguza uzito wao. Mambo ya kuitana Big Dady (jibaba), Big Mama (jimama) na hata tabia ya watu weusi kupenda wanawake wanene ni sababu za kitamaduni zinazochangia ufutufutu kwa watu weusi.

Wanawake weusi ndiyo wanaongoza zaidi katika unene huu wa futufutu wakifuatiwa na wanaume na halafu watoto. Jimbo la Maine ndilo linaongoza kwa kuwa na watu weusi futufutu wengi zaidi (asilimia 45). Kwa habari zaidi soma hapa.

Niliposoma utafiti huu nilifikiri mambo mawili. Kwanza, kwa nini unene huku ni dalili ya umasikini wakati sisi kule nyumbani ni

No comments: