Wednesday 1 July 2015

NILIMPENDA SANA MCHUMBA WANGU, LAKINI MWISHONI AMEBADIRIKA ANANICHUKIA SANA, ANACHUKIA HADI NDUGU ZANGU NAOMBENI MNISHARI NIFANYAJE NA BADO NAMPENDA SANA

Natumai uumziwa vzur dada Violet. Me nikajana mwenye 23yrs nipo dar. Bilashaka natumai utakua ni jibu la tatizo langu. Hapo awali nilikua na rafik ya wakike ambae kwa dhat mimi nilikua na mpenda sana, kama unavyojua mapenz kikohoz hakifichiki. Nilikua namuonesha dalili za waz kuwa nampenda huku nikishindwa Kumwambia kwan yeye alionesha kuniheshimu sana. Sasa siku 1 katka story zetu akanambia kua yeye ana mume na pia ana mtoto m1, lkn mumewe yupo nje kimasomo. Kwa kweli hili lilinifanya nirudi nyuma katka mchakato wangu wakutaka kumwambia ukwel kuhusu kumpenda yeye.
 Lkn ckusita nikaulizia zaid kwa shoga zake kuhusu kuolewa kwake. Kwa bahat nzur wakanambia ukwel kuwa hajaolewa na amekudanganya tu. Sasa mimi baada ya kuona hv nikaona anampango wa kuzuia ishara zangu za mapenz kwake. Na hatimaye nikaona ni bora ni mueleze ukweli kuhusu moyo wangu. Sasa siwez japo najua hajaolewa, lkn nikatumia trik hii: 
nikamwambia kuwa katka sikuzote za urafiki wetu nimekua ninajambo moyon mwangu nataka nikueleze lkn cwez kwan we umeolewa. Akanambia hv mimi cjaolewa nilikua nakudanganya tu, Hapo hapo ckusubir hil wala lile nikaanza kumueleezea hali ya moyo wangu juu yake ie nampenda sana. Kwakwel yeye hakusema chochote kwa wakati ule yaan mimi ndio nilikua naongea mwanzo mwisho. 
Sikumuacha hiv hiv bal nilivua pete yangu nakumvisha yeye jambo ambalo lilinifanya nijihakikishe kuwa amekua wangu, baada ya hapo tukaagana vzur tu! nakuendelea na mambo mengine. Lkn chakushangaza tena chakushangaza tangu hapo alianza kunichukia vibaya mno, alichukia hadi wazazi wangu wakat hapo mwanzo aliwapenda sana pindi nilivyo kua nae kama rafik. Kwakwel dada violet ananichukia mpaka namuogopa. 
Sijui nn kimetokea, yaan salamu haitikii. Nahitaji mawazo yako dada Violet kwan nampenda sana tena sana sanna. unadhan kwanin amekuhiv ananichukia? 
PEKE YANGU SIWEZI KUJIBU WAPENZI,,, NAOMBENI TUSAIDIE KUMJIBU MDOGO WETU SOTE......

No comments: